Tazama Makali ya Simba na Yanga

Baada ya kusimama kwa muda Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwaajili ya kupisha michezo ya kalenda ya FIFA huku baadhi ya wachezaji wakienda kuziwakilisha timu zao za taifa.

Tayari klabu mbali mbali zinazoshiriki ligi kuu zimeanza kurejea katika mazoezi kujiweka sawa kwaajili ya michezo inayowakabili.
Huko Msimbazi, Simba SC imeanza kujiweka sawa kwaajilia ya kukipiga na Mtibwa Sugar.
Wakati klabua ya Young Africans imeanza mazoezi yake leo kwaajili ya kujiweka sawa na mchezo ujao wa ugenini dhidi ya Kagera Sugar katika dimba la Kaitaba.
Mabingwa hao wa kihistoria wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara wamejifua katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
Kwa sasa Simba ipo kileleni kwenye msimamo wa Ligi Kuu Vodacom Tanzania bara kwa alama 11 ikifuatiwa na Mtibwa Sugar na Azam FC zote zikiwa na alama 11 ikiwa tofauti ni magoli ya kufungwa na kufunga

No comments: