Mavazi ya niqab na burka yapigwa marufuku Austria


File pic of Swiss woman in a niqabHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionSheria ya kupiga marufuku niqab na burka nchini Autralia yatekelezwa
Sheria inayoiga marufuku vazi la kiislamu katika sehemu za umma imeanza kutekelezwa nchini Austria.
Serikali inasema kuwa sheria hiyo inayosema kwa uso lazima uonekane ni ya kulinda tamaduni za Austria.
Inakuja kabla ya uchaguzi mkuu baadaye mwezi huu ambapo chama cha mrengo wa kulia cha Freedom kinatarajiwa kupata mafanikio.
Makundi ya waislamu yamekosoa sheria hiyo yakisema kuwa ni watu wachache waislamu nchini Austria ambao huvaa Niqab
Sheria inapiga marufuku mavazi ya kiislamu kama burka na Niqab.
Takriban wanawake 150 huvaa burka nchini Austria lakini maafisa wa kitalii wanasema kuwa hatua hizo pia zitawazuia wageni kutoka nchi za Ghuba.
Ufaransa na Ubelgiji zilipiga marufuku vazi la burk mwaka 2011 na hatua kama hiyo kwa sasa inazungumziwa katika bunge la Uholanzi.
Chansela wa Ujerumani Angela Merkel amesema kuwa vazi la kufunika uso wote litapigwa marufuku nchini Ujerumani

Tofauti kati ya vazi la niqab na burka

Woman wearing a Niqab
Image captionNiqab
Woman wearing a Burka
Image captionBurka

No comments: