Rais John Magufuli azushiwa siku ya kuzaliwa Kwenye mitandao ya kijamii

Msemaji wa Ikulu, Gerson Msigwa amekanusha taarifa ambazo zimezagaa katika mitandao ya kijamii kuwa
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amezaliwa tarehe 10.10.2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe
Magufuli
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na msemaji wa Ikulu, imesema Rais Magufuli amezaliwa tarehe 29.10.1959 huko mkoani Chato.

“Taarifa zinazoenezwa kuwa leo tarehe 10.10 ni siku ya kuzaliwa kwa Rais Magufuli sio kweli. Mhe. Dkt John P.J. Magufuli alizaliwa 29.10.1959,” alitweet Msigwa kupitia mtandao wa Twitter.
Hata hivyo baada ya mesemaji huyo kutoa taarifa hiyo, baadhi ya mashabiki katika mtandao huo wamelishangaa tukio hiko la aina yake kwa kuwa taarifa za siku ya kuzaliwa ya rais ni rahisi kupatika mtandaoni.

No comments: