Aliyekuwa rais wa Iraq aaga dunia


Aliyekuwa Rais wa Iraqi na kiongozi mkuu wa Wakurdi, Jalal Talabani, amefariki.
Image captionAliyekuwa Rais wa Iraqi na kiongozi mkuu wa Wakurdi, Jalal Talabani, amefariki.
Aliyekuwa Rais wa Iraqi na kiongozi mkuu wa Wakurdi, Jalal Talabani, amefariki.
Talabani ameaga dunia huko Ujerumani, akiwa na umri wa miaka 83.
Aliingia kwa mara ya kwanza katika siasa za Wakurdi akiwa kijana mdogo na akapanda ngazi hadi kufikia ngazi ya juu kwenye uongozi wa kundi la Wakurdi pamoja na kiongozi nchini Iraq kupitia hatua ya ugawanaji mamlaka, baada ya kupinduliwa kwa hayati Rais Saddam Hussein.
Kama Rais, Bwana Talabani aliamua kutumika kama muunganishi mkuu, kwa Wairaqi wote, na pia kujaribu kurejesha uhusiano mzuri na mataifa jirani.
Aliunga mkono juhudi za Marekani kuivamia Iraq.

No comments: