Picha,Wenger akimkabidhi zawadi Gareth Barry baada ya kuweka rekodi ya kucheza game nyingi zaidi kwenye EPL

Kiungo Gareth Barry Wa klabu ya West Brom jana amecheza mechi dhidi ya Arsenal iliyomfanya aweke rekodi ya kuwa mchezaji anayeongoza kwa kucheza mechi nyingi za ligi kuu nchini Uingereza kuliko mchezaji mwingine yoyote.
Amecheza mechi 633 na kuvunja rekodi ya Ryan Giggs aliyecheza mechi 632.
Baada ya mechi ya jana ambayo West Brom walipigwa 2-0, kocha Arsene Wenger alimkabidhi kiungo huyo zawadi ya jezi iliyoandikwa 633 kumpongeza kwa kuweka rekodi hiyo.

No comments: