Beyonce kutoa mapato yote ya remix ya wimbo Mi Gente kusaidia watu Puerto Rico.

Staa wa muziki nchini Marekani Beyonce amesema atatoa pesa zote zitakazopatikana kwenye mauzo ya Remix ya wimbo wa  J Balvin na Willy William Ft Beyonce -Mi Gente,  kusaidia walioathirika na Kimbunga cha MARIA katika visiwa vya Puerto Rico.
Beyonce kaimba kwa Lugha tatu kwenye wimbo huu ambazo ni Spanish, French na English.
Kwenye Instagram yake aliandika “I am donating my proceeds from this song to hurricane relief charities for Puerto Rico, Mexico and the other affected Caribbean islands,”
Remix hii ya J Balvin na Willy William Ft Beyonce -Mi Gente imetazamwa na watu 100,000 ndani ya dakika 30 kwenye mtandao wa YouTube
Pia kwenye mashairi ya wimbo huu Beyonce ana taja waathirika wa vimbunga hivyo“Lift up your people/ From Texas to Puerto Rico/ Dem islands to Mexico.”

No comments: