Mwigizaji Jamie Foxx ametajwa kuigiza kwenye filamu ya maisha ya bondia Mike Tyson

.
Muigizaji, Mwimbaji na Mchekeshaji  maarufu duniani Jamie Foxx ameripotiwa kukubali dili la kuigiza kama Mike Tyson kwenye filamu ya Bondia huyu maarufu na mwenye ushawishi mkubwa.
Tyson ambaye ni bingwa wa ngumi za kulipwa  wa uzito wa juu duniani, amethibitisha stori hii na kusema Jamie Foxx tayari amesaini dili hilo, na utaratibu wa kuanza ku-shoot utaanza siku zijazo sababu Jamie Foxx alikuwa akivizia dili hili toka mwaka 2014.
Filamu hii itaonyesha maisha halisi ya Tyson tangu utoto, alipokwenda jela kwa miaka mitatu (1992-95) kwa kosa la Ubakaji, mpaka kujizolea umaarufu kupitia mchezo wa masumbwi.
Tyson pia amesema anaimani watu hawata ipenda filamu hio sababu yeye ana historia mbaya ya maisha yake.

No comments: