Hofu ya kulipuka volkano katika kisiwa cha kitalii cha Bali

Image result for bali island photo
Indonesia imeonya kuwa mlima wa volcakano katika kisia cha kitalii cha Bali umefikia kiwango kibaya huku kukiwa na hofu ya kutokea kwa mlipuko ya volkano.
Mamia ya mitetemeko midogo ya ardhi imerekodiwa siku ya Jumatatu kwenye mlima Agung ishara ya kutokea kwa mlipuko wa volkano.

Lakini maafisa wanasisitiza kuwa huwawezi kutabiri ni lini mlima huo unaweza kulipuka.
Zaidi ya watu 75,000 wanaoishi karibu na mlima huo wamehamishwa kutoka makwao, na eneo hilo sasa liko chini ya tahadhari kubwa ya volkano.
A view of Mount Agung on September 24, 2017 in Karangasem regency, Island of Bali,

Hofu ya kulipuka volkano katika kisiwa cha kitalii cha Bali
Msemaji wa shirika la taifa la majanga nchini Indonesia Sutopo Purwo Nugroho aliwaambia waandishi wa habari siku ya Jumatatu kuwa mlima dalili zinaendelea kuongezeka.
Alisema kuwa kuna uwezekano mkubwa kuwa mlima huo utalipuka, lakini akasema kuwa haijulikana mlima huo utalipuka lini.

Villagers rests at a temporary evacuation centre, for people living near Mount Agung, a volcano on the highest alert level, inside a sports arena in Klungkung, on the resort island of Bali, Indonesia, 24 September 2017 in this photo taken by Antara Foto.Haki miliki ya pichaREUTERS

Maeneo kuu ya kitalii ya Kuta na Seminyak, yaliayokaribu kilomita 70 kutoka mlima huo hayajaathiriwa kwa sasa na safari za ndege zinaendelea kama kawaida.
Lakini nchi kadha zikiwemo Uingereza, Ausralia na Singapore zimetoa onyo la kusafiri kwa raia wao zikionya kuwa huenda kukawa na tatiza ya safari za ndege.
Zaidi ya watu 1000 waliuawa wakati mlima Agung ulilipuka mwaka 1963.

No comments: