Makatibu tawala wa mikoa watakiwa kusimamia upatikanaji wa malipo ya muda wa ziada ya wauguzi.


Na.Ahmad Mmow.
MAKATIBU tawala wa mikoa(RAS's) nchini wameagizwa kufuatilia, kusimamia na kuhakikisha wauguzi wanalipwa madai yao yote yanayotokana na kazi walizofanya nje ya muda uliopo kisheria.
Agizo hilo limetolewa leo na waziri mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,Kassim Majaliwa(MB) alipozungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa wauguzi na kongamano la kisayansi uliofanyika leo katika manispaa ya Lindi.
Na.Ahmad Mmow.
MAKATIBU tawala wa mikoa(RAS's) nchini wameagizwa kufuatilia, kusimamia na kuhakikisha wauguzi wanalipwa madai yao yote yanayotokana na kazi walizofanya nje ya muda uliopo kisheria.
Agizo hilo limetolewa leo na waziri mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,Kassim Majaliwa(MB) alipozungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa wauguzi na kongamano la kisayansi uliofanyika leo katika manispaa ya Lindi.


Majaliwa alisema taaluma za uuguzi na udaktari zinamisingi na taratibu zake ambazo zinatakiwa kufuatwa na kuheshimiwa. Hivyo yeyote ambae hataki kuziheshimu taratibu hizo hanabudi kuchukuliwa hatua
"Viongozi lazima wazingatie sheria,kanuni na taratibu.Yapo mabaraza yanaouwezo wakubaini ukubwa wakosa,nihatua gani zichukuliwe na nani wanapaswa kuchukua hatua.Kwahiyo mabaraza yashirikishwe na yatumike ili yatambue hatua zinachukuliwa kwa watumishi hao kwenye maeneo yake,"alisisitiza Majaliwa.
Aidha alitoa wito kwa wauguzi kufanya kazi kwa uadilifu kwa kuzingatia viapo vya kazi hiyo.Ikiwamo kuepuka lugha chafu na kali kwa wagonjwa,rushwa na dharau

No comments: