Mahakamani tena vigogo wa simba tazama utetezi wao


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirisha kesi ya utakatishaji fedha na kugushi inayowakabili Rais wa Simba, Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ hadi October 11, 2017 kwa sababu upelelezi haujakamilika.
Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Leornad Swai amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa kuwa shauri hilo limeitishwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi haujakamilika, hivyo anaomba ipangiwe tarehe nyingine ambapo baada ya kueleza hayo Hakimu Mwambapa aliahirisha kesi hiyo hadi October 11, 2017.
Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha Dola za kimarekani 300,000.
Washtakiwa wapo rumande kwa sababu shtaka la kutakatisha fedha linalowakabili halina dhamana.

No comments: