Punda amezea mate gari lenye rangi ya karoti

Gari la McClaren Spider na punda
Mahakama ya Ujerumani Alhamisi itaamua Alhamisi iwapo mmiliki wa punda aliyejaribu kulitafuna gari anapswa kulipia gharama za uharibifu wa gari hilo.
Mnamo Septemba 15 mwaka jana, Markus Zahn aliliegesha gari lake kwenye eneo linalopakana na uwanja alikowekwa punda huko Vogelsberg, wiliya iliopo kwenye jimb la Hesse Ujerumani.
Punda kwa jina Vitus aliitafuna sehemu ya nyuma ya gari hilo, anasema.
Polisi wanaeleza huenda Vitus alidhani gari hilo ni karoti.
Farasi na punda katika uchaguzi wa urais Kenya
Lakini mmiliki wa punda huyo anapinga tuhuma hizo na badala yake anaitisha €6,000 kulipia gharama za uharibifu.
Anasema huenda Vitus hakufanya hilo na kwamba bwana Zahn hange egesha gari lake linalodiawa kuwa na thamani ya Euro 300,000 - karibu na uwanja huo.
Mahakama ya kiraia ya Giessen inatarajiwa kutoa uamuzi katika kesi iliyogubika vyombo vya habari kitaifa.

No comments: