Mbunge Akiri Kukojoa Hadharani Mbele za Watu

Mbunge kutoka nchini Uganda, Ibrahim Abiriga amekiri kuwa alikojoa hadharani katika uzio wa Wizara ya Fedha baada ya kubanwa na mkojo.

Jana nilikuwa nimebanwa sana, nikaenda kukojoa, alisema Abiriga wakati akifanya mahojiano na na kituo cha runinga cha nbs.

Alipoulizwa na mwandishi wa habari kwanini alifanya hivyo wakati ofisi za bunge zilikuwa jirani, alijibu kwa mshangao, akiuliza kwanini asifanye hivyo, kwanini abane mkojo?

Mbunge hiyo ni miongoni mwa wabunge wanaounga mkono kuondolewa kwa kipengele cha ukomo wa umri wa Rais ili kumruhusu Rais Museveni kugombea tena katika uchaguzi wa mwaka 2021.

Katiba ya Kenya hairuhusu mtu anayegombea Urais kuwa na umri zaidi ya miaka 75, ambapo kama katiba haitobadilishwa, Museveni hatoweza kugombea tena kwani atakuwa amezidi miaka hiyo.

No comments: