Mwanzilishi wa jarida la Playboy afariki dunia

Muanzilishi wa jarida la Playboy Hugh Hefner
Hugh Hefner, mwanzilishi wa jarida la kimataifa la watu wazima - Playboy, amefariki akiwa na umri wa miaka 91.
Playboy Enterprises Inc imesema alifariki kwa amani nyumbani .
Hefner alianza kuchapisha jarida hilo jikoni nyumbani mwake mnamo 1953. Likawa jarida linalo uzika zaidi la wanaume duniani.
Cooper Hefner, mwanawe amesema "atakumbukwa kwa ukubwa na wengi".
Alimtaja babake kama "Mojawapo ya watu wa kwanza kujitosa katika uandishi na aliishi maisha ya aina yake na yenye utofuati," na amemuita mtu anayetetea uhuru wa kuzungumza, haki za kiraia na uhuru wa kijinsia.
Hugh Hefner Crystal Harris, 2011
Jarida la Hefner lilichangia kile kinachoonekana kuwa kuheshimiwa kwa picha za utupu katika vyombo vya habari na hilo lilimtajirisha na kumfanya kuwa milionea.
Ufanisi wake ukamuezesha kufungua maenoe ya kucheza kamari na vilabu vya burudani.
Tajiri huyo aliyeonekana mara nyingi akivaa nguo za hariri, aliishi maisha ya starehe, akiwachumbia na kuwaoa wanamitindo wanaopigwa picha katika jarida hilo .
Katika miaka yake ya baadaye alifurahikia kuandaa tamasha kubwa na mikusanyiko ya starehe katika majumba yake ya kifaharai.
Anadai kulala na zaidi ya wanawake 1000 na amesifia nguvu zake kwa dawa za kuongeza nguvu za kiume Viagra.

No comments: