Hizi hapa dondoo za usajili Ulaya leo 4/10/2017



Klabu ya Chelsea inaangalia kuwasajili Alex Sandro na Alexis Sanchez ilikuendelea kumbakisha Antonio Conte klabuni hapo.
Arsenal inajiandaa kumuuza Theo Walcott mwezi Januari.
Willian ameivunja moyo klabu ya Manchester United iliyokuwa na matumaini ya kumsajili kwani hafikirii kuihama Chelsea.
Mshambuliaji wa Liverpool, Danny Ings yupo njiani kujiunga na Leeds United mwezi Januari.
Taarifa zinaeleza kwamba Manchester United ipo tayari kumsajili nyota wa Arsenal, Mesut Ozil kwa uhamisho huru katika majira ya kiangazi yajayo.
DONDOO MBALIMBALI ZA MICHEZO ULAYA.
Kiungo wa Manchester United, Paul Pogba amezuiwa kucheza mpira wa kikapu ili kuondoa hofu ya kuweza kuwa na majeraha zaidi.
Huenda kocha wa Chelsea, Antonio Conte akaihama klabu hiyo na kutimkia AC Millan mwishoni mwa msimu huu.
Everton wanaangia mbadala wa kuchukua nafasi ya kocha wao, Ronald Koeman huku wakitarajia kumpa timu kwa muda Walter Mazzarri.
Mmiliki mwenye hisa nyingi kwenye klabu ya Arsenal, Stan Kroenke, ana dili linalokaribia pauni milioni 525 kununua hisa za Alisher Usmanov, mmiliki anayeshilikilia nafasi ya pili kwa kuwa na hisanyingi klabuni hapo.

No comments: