Dharau za Samatta mbele ya malawi soma ufurahi

Nahodha wa Taifa Stars , Mbwana Samatta amesema kuanza kupewa nafasi kwa wachezaji wa Kitanzania wanaocheza nje kutaisaidia Stars kufanya vizuri kwenye michezo ya Kimataifa.


Stars itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Malawi leo kwenye Uwanja wa Uhuru katika kujiandaa na kusaka kufuzu kwa mashindano ya mataifa ya Afrika 2019, Cameroon .
Mshambuliaji wa KRC Genk ya Ubelgiji, Samatta alisema wachezaji wamekuwa wakijituma, lakini uzoefu wa michezo ya kimataifa unaweza kusaidia sana kwenye michezo ya kuwania nafasi za AFCON, bado tunayo nafasi ya kufanya vizuri,”
“Tuendelee kumuamini mwalimu ili afanye kazi yake, kwenye hata hii michezo ya kirafiki tunayocheza inakijenga kikosi kuzoeana na hata kupata uzoefu pia wa mechi za kimataifa,” alisema Samatta.
"Ni wakati wa soka la Tanzania kupiga hatua kisoka ili kuhakikisha hilo ni kupata matokeo ya ushindi kwenye mechi kama hizi za kirafika na kufuzu mashindano yoyote yaliyokuwa mbele yetu," alisema Samatta.

No comments: