Davido azigawa tuzo za Afrimma


Baada ya kupokea ushindi wa tuzo za muziki za Africa Muzik Magazine Awards & Music Festival (AFRIMMA), Davido ametoa ushindi huo mnono kwa rafiki yake Tagbo na DJ Olu waliofariki wiki kadhaa zilizopita.


Davido ambaye ameshinda tuzo mbili katika kipengere cha ‘Artist of the Year’ na ‘Song of the Year’ kupitia ngoma ya “IF” ametoa ushindi huo mnono kama ishara ya kuwaenzi wapendwa wake hao.
“One for Olu , One for Tagbo ! Nothing but love , support , and positive energy came from you guys ! Thanks for you guys for keeping me motivated . This is ‘OUR’ Award. Thank you Afrimma ! Thank you Lord,” ameandika Davido katika ukurasa wake wa Instagram.
Baada ya kutokea vifo vya watu hao msanii huyo alishutumiwa na baadhi ya watu kuhusikia na sakata hilo hata hivyo Davido alilipinga vikali.



No comments: