Wanawake wa Tanzania kukabiliana na Nigeria


Tanzania
Image captionTimu ya soka ya taifa ya wanawake chini ya umri wa miaka 20 wakiwa na viongozi wao
Timu ya soka ya taifa ya wanawake chini ya umri wa miaka 20 ya Nigeria inatarajiwa kutua jijini Dar es salaam leo ijumaa ikiwa na kikosi cha watu 31 .
Timu hiyo inataraji kucheza na Tanzania 'Tanzanite' mchezo wa marudiano kuwania kucheza fainali za Kombe la Dunia 2018 nchini Ufaransa .
Mchezo huo utafanyika Jumapili Oktoba mosi Uwanja wa Chamazi nje ya jiji la Dar es Salaam, Mchezo wa Awali Tanzania ilipoteza kwa kufungwa mabao 3-0 nchini Nigeria.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewapa fursa mashabiki wengi kuingia uwanjani kuishangilia timu yao ya taifa The Tanzanite.

No comments: