Umoja wa mataifa wazuiwa kufanya ziara Rakhine nchini Myanmar

Umoja wa mataifa unasema kuwa, utawala wa Burma umefutilia mbali mipango ya Umoja huo kuzuru jimbo la Rakhine nchini Myanmar.

Hilo ni eneo ambalo kulishuhudiwa idadi kubwa zaidi ya watu wa jamii ndogo ya waislamu Wa- Rohingya, waliotoroka makaazi yao kuepuka mapigano.

Msemaji wa Umoja wa mataifa huko Yangon, Stanislav Saling, ameiambia BBC kuwa hakuna sababu zozote ambazo zilitolewa kuhusiana na hatua ya kuwazuia maafisa wa Umoja wa mataifa kuzuru maeneo hayo.

Umoja wa mataifa umekuwa ukishinikiza kuruhusiwa kulizuru jimbo hilo la Rakhine, ili kupeleleza kiini cha Warohingya hao kuhama kwa wingi kutoka maeneo hayo, kuanzia mapema mwezi uliopita.

Makumi kwa maelfu ya waislamu, Wabudha na Wahindu wanaishi katika majengo ya muda katika jimbo hilo la Rakhine tangu kuanza kwa mashambulio yaliyokuwa yakitekelezwa na warohingya wenye itikadi kali.

Hatua iliyosababisha Jeshi la Myanmar kuanza kuwashambulia Warohingya

No comments: