Harufu ya bangi kwenye gari ya Young Thug yamletea matatizo makubwa zaidi.

Rapa Young Thug anazidi kuogeza matatizo ya kisheria kwenye mkanda wake baada ya kukamatwa na Marijuana hivi karibuni.
Young Thug alikamatwa weekend hii mjini Georgia kwa kosa la kuwa na gari yenye Tinted kwenye vioo vyote na ndipo polisi walipohisi harufu ya bangi kwenye gari hio aina ya Maybach.
Baada ya msako wakiwa na sababu ya Harufu, Polisi walikuta Misokoto miwili ya BangiDawa za kulevyaBunduki Mbili, na dola 50000.
Kwa sasa Young Thug anakabiliwa na mashtaka ya kukamatwa na silaha bila kibali, kutembea na bangi na kukutwa na dawa za kulevya
Pia Young Thug alifunguliwa mashtaka ya kuendesha gari yenye Tinted kwenye vioo vyote, Jumatano hii aliwekewa dhamana na sasa yuko nje.

No comments: