Paris St-Germain watoka sare na Montpelleir, Neymar akiwa nje


Paris St-Germain ilipoteza alama katika ligi ya kwanza kwa mara ya kwanza msimu huu, bila ya kuwepo Neymar walipotoka sare ya sufuri na Montpelleir.

Neymar ambaye alitofautiana na Edinson Cavani kuhusu ni nani angepiga penalti katika mechi yao ya mwisho na Lyon, anaaminiwa kuwa na jeraha dogo la mguu.

Kylina Mbappe aliokoa mara mbili kutoka kwa Benjamin Lecomte lakini pia mchezo wa PSG haukuwa mzuri.

Kwa sasa wako pointi moja juu ya mabingwa Monaco ambao waliwapa kichapo cha mabao 4-0 Lille siku ya Ijumaa.

No comments: